Tuesday, February 27, 2018

Aida olomi wenzake kufikishwa mahakamani Leo baada ya mahakama Mkuu kungilia

Anaandika waliki  Alex massaba

Nipenda kuwapa taarifa juu ya watu wetu watatu (Aida Olomi, Isaack lomanus, na Erick John) wanaoshikiliwa na jeshi la polisi katika kituo cha polisi cha osterbay, jijini Dar es salaam kwa takribani siku 11 sasa, na kwa muda wote huo polisi imewanyima dhamana.

Timu ya Mawakili tuliamua kufungua kesi Mahakama Kuu kuwashitaki IGP na Mwanasheria Mkuu (AG) kwa kosa la kuendelea kuwashikilia wateja wetu kinyume na Sheria za nchi. Mbaya kuliko lote hawana kibali chochote kutoka kwa hakimu cha kuendelea kukaa nao kituoni.

Tumshukuru mwenyezi Mungu kuwa hatua hii ya Mahakama Kuu tumefanikiwa kupata summons na tumemsave IGP na AG, ambapo kesi imepangwa kusikilizwa kesho SAA saba mchana Mbele ya Jaji Arufani. 

Aidha, kuna taarifa kuwa polisi wanajiandaa kuwapeleka Mahakamani Kisutu mida ya asubuhi kwa siri ili kukwepa waandishi Wa Habari.

Niwaombe makamanda wote kesho kuazia asubuhi tujitokeze kwa wingi na niombe tugawanyike wengine tuanzie osterbay Polisi na wengine tutangulie Mahakamani Kisutu.

Swala la wadhamini naomba lipewe kipaumbele ni aibu kubwa sana tunapofanyakazi kubwa na ngumu ya kuwezesha watu wetu kufikishwa Mahakamani halafu wanakosa wadhamini. Naomba madiwani wetu wajitokeze kwa wingi.

Aidha, kuna taarifa kuwa serikali wanajipanga kuja na kiapo cha kuzuia dhamana ya watu wetu, sisi Mawakili tumejipanga kupambana na hilo.

Zaidi ya yote nawashukuru watu wote kwa namna ambapo kila mmoja wetu amepambana kuhakikisha kwamba wenzetu hawa wanakuwa huru na Mungu akipenda muda mfupi ujao tutakuwa na uraiani.

Wakili Alex Massaba
27/02/2018








My take: za kuambiwa changanya na za kwako


No comments:

Post a Comment

UHABA WA MAJI MOROGORO: Mama apambana na mamba, anusurika kuliwa, apoteza mwanae.

Siku sita kabla ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake  Duniani, mwanamke mmoja amenusurika kuliwa na mamba wakati akiteka maji kwenye Mto Mget...