Wednesday, February 28, 2018

UTARATIBU WA MKATOLIKI AINGIAPO HADI ATOKAPO KANISANI


  •  Ninapoingia kanisani nachovya maji ya baraka na kusema

"Unitakase Ee Bwana mimi na uovu wangu wote, ili nipate kustahili kushiriki ibada takatifu' Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu" Amina! 




  • Ninapiga goti huku nikisema"Mungu wangu na Bwana wangu"

  • Nikiinuka nasema

"Nitakusifu na kukuabudu katika Ekaristi takatifu"

  • Naenda mpaka kwenye bench, napiga magoti au nakaa nikiwa mimeinamisha kichwa (kama mabenchi yameisha nabaki nimejisimamia) huku nikitoa nia yangu ya kusali misa siku hiyo, mfano

"Ee Mungu, ninaungana nawe na jeshi lote la mbinguni, pamoja na Mama Bikira Maria, nikiwa na nia ya kumwombea mama yangu ambaye ni mgonjwa, jirani yangu ambaye mpaka sasa hatuelewani na pia familia yetu ambayo haina amani, Mungu kupitia misa hii rejesha hali ya mama yangu, rejesha uelewano na jirani yangu, na pia rejesha amani ya familia yetu pamoja na familia zote ambazo hazina amani"

  • Ninaendelea na misa na Kushiriki litrujia kikamilifu

  • Mwisho wakati wa kuondoka nachovya maji ya baraka nikisema

"Unilinde Ee Mwenyezi Mungu, nikapate kuwa mfano katika jamii yangu, na nikushuhudie katika matendo yangu"
(Hapo nachovya maji ya baraka na kufanya ishara ya msalaba) "Kwa jina la Baba na la Mwana na la RohoMtakatifu, amina"


No comments:

Post a Comment

UHABA WA MAJI MOROGORO: Mama apambana na mamba, anusurika kuliwa, apoteza mwanae.

Siku sita kabla ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake  Duniani, mwanamke mmoja amenusurika kuliwa na mamba wakati akiteka maji kwenye Mto Mget...