Wednesday, February 28, 2018

PAMBANIENI UHURU: anaandika baba askofu Steven Munga

Uhuru si zawadi tunayopewa na watawala bali ni haki ya asili ya kilamtu kwa sababu tuliumbwa nayo. NI HAKI YA ASILI!!! 

Kiuhalisia tawala za kidunia maranyingi hulenga katika kupora uhuruhuo ili wawatawale watu kamawapendavyo. Lakini hivyo si sawa. Hata Mungu alipowaumba Adamu na Hawa aliwapa uhuru wa kutosha wa kufanya maamuzi na uchaguzi (Mwanzo mlango wa 1 na wa 2). 

Ni ubaya na uovu pale tu uhuru huo unapotumika vibaya kwa lengo la kuingilia, kukandamiza na kuhatarisha uhuru na maisha ya wengine. Hii ndio sababu zipo katiba na sheria za nchi huru pamoja na maazimio ya kimataifa vinavyotungwa ili kulinda uhuru huo. 

Uhuru wetu ni haki na kipawa chaasili tulichopewa na muumba wetu
Ni wajibu wako kupambana na yeyote anayejaribu kukunyang'anya uhuruwako ambao ni haki yako ya asili.

No comments:

Post a Comment

UHABA WA MAJI MOROGORO: Mama apambana na mamba, anusurika kuliwa, apoteza mwanae.

Siku sita kabla ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake  Duniani, mwanamke mmoja amenusurika kuliwa na mamba wakati akiteka maji kwenye Mto Mget...